CHANGAMOTO ZA MATUMIZI YA KIWANJA

Watu wengi wamekuwa wakikutana na changamoto za kusumbuliwa na mamlaka hasa halmashauri za miji, manispaa na majiji pale wanapokuwa wanafuatilia vibali vya ujenzi kutokana na suala zima la kigezo cha matumizi ya kiwanja.

WATU WENGI WAMEKUWA WAKIKUTANA NA CHANGAMOTO ZA MATUMIZI YA KIWANJA WANAPOFUATILIA KIBALI CHA UJENZI

Mara nyingi hasa miaka ya hivi karibuni kupata kibali cha ujenzi wa eneo lako suala la matumizi ya kiwanja limekuwa ni changamoto kubwa sana kwa baadhi ya watu kwa sababu kuna matumizi ya kiwanja yanayokaribiana sana kiasi kwamba mtu unaweza kufikiri uko sahihi na bado ukajikuta unazuiliwa. Kumekuwa kuna utofauti mdogo sana kati ya matumizi ya kiwanja kwa makazi biashara na makazi ya kawaida na hivyo unaweza kupeleka michoro ambayo ni makazi ya kawaida na bado ikaonekana kwamba ni makazi baishara, kitu ambacho kitakupa wakati mgumu.

BADO KUMEENDELEA KUWEPO NA UTATA JUU YA USAHIHI WA VIGEZO VYA MATUMIZI YA JENGO

Hivyo ni muhimu zaidi kuwa makini tangu mwanzoni au kufanya kazi na mtu anayeelewa vizuri usumbufu uliopo kwenye suala la matumizi ya kiwanja na hata vigezo vingine vya kiwanja kuendana na aina ya jengo/majengo unayotaka kujenga katika kiwanja husika vinavyoweza kukupunguzia usumbufu wakati unafanya ufuatiliaji wa kibali cha ujenzi.

UMAKINI UNAHITAJIKA ILA KUPUNGUZA USUMBUFU UNAOTOKANA NA MATUMIZI SAHIHI YA KIWANJA WAKATI WA KUFUATILIA KIBALI CHA UJENZI

Architect Sebastian Moshi

Whatsapp/Call +255717452790

0 replies

Leave a Reply

Want to join the discussion?
Feel free to contribute!

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *