TENGENEZA BUSTANI NZURI KUONGEZA THAMANI YA NYUMBA NA MANDHARI YAKE.

Utengenezaji wa bustani kwa sababu za mbalimbali ikiwemo kuboresha na kupendeza mazingira ni jamba ambalo limekuwa likifanyika tangu zamani za kale. Mpangilio wa kujenga mistari ya mawe(kerbstones) na vigae vya tofali za ardhini(paving blocks) kama ardhi ngumu pamoja na upandaji miti kwa mpangilio sahihi uliotengenezwa kwenye ramani huongeza mvuto na thamani ya nyumba na mandhari yake kwa kiasi kikubwa sana.

BUSTANI NI MPANGILIO MCHANGANYIKO UNAOLETA ASILI YENYE KUVUTIA

Mandhari inayozunguka nyumba hujumuisha maeneo yenye ardhi ngumu(hard landscape) kama vile njia za gari na za miguu, parking za gari, eneo la kupumzika maarufu kama “gazebo” n.k., ardhi laini(soft landscape) ambayo hujumuisha maeneo yenye bustani za nyasi, maua, miti ya kivuli, miti ya matunda, mbogamboga na maeneo mengine yote yenye kijani kibichi, maji(water landscape) ambayo hujumuisha bwawa la kuogelea(swimming pool), bwawa la samaki, mifereji ya umwagiliaji, maji yanayoruka n.k.,. Mjumuiko wa haya katika mpangilio sahihi wa eneo la kiwanja linalozunguka nyumba huongeza sana thamani ya nyumba na kuboresha sana mandhari inayozunguka nyumba.

UKIJENGA BUSTANI KWA USAHIHI UTAIFURAHIA ZAIDI NYUMBA YAKO

Jambo la muhimu sana ni kwamba yote haya yanapaswa kuanza na michoro ya ramani kabla ya utekelezaji. Unapotanguliza utekelezaji kabla au bila ya michoro ya ramani ya bustani na mandhari yote ya nyumba pamoja na mahusiano yake na nyumba yenyewe unajiandaa kukutana na changamoto sana na mwisho wa siku ubora wa kazi utakuwa wa viwango vya chini sana tofauti na ikiwa utaanza na ramani au pengine ukafeli kabisa.

BUSTANI KUPANGILIKA KWA USAHIHI INAHITAJI KUANZA NA MICHORO YA RAMANI KABLA YA UTEKELEZAJI

Tumia bustani na mpangilio sahihi wa mandhari inayozunguka nyumba kuongeza sana thamani ya nyumba yako.

Architect Sebastian Moshi.

Whatsapp/Call +255717452790.

4 replies

Leave a Reply

Want to join the discussion?
Feel free to contribute!

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *