MKANDARASI ANAPASWA AWE NA WASHAURI WA KITAALAMU ILI ASIHARIBU KAZI.

Kazi yoyote ili ifanyike kwa usahihi na kwa viwango vya juu inahitaji wataalamu waliobobea katika fani husika kushiriki na kutoa ushauri wa kitaalamu katika kufanikisha kwa viwango sahihi na vinavyotarajiwa kile ambacho kinafanyika. Hili ni suala linafanya kazi katika fani zote na katika kazi za miradi yote hasa miradi mikubwa.

WATAALAMU WALIOBOBEA KWENYE TAALUMA HUONGEZA THAMANI YA MRADI KWA VIWANGO VYA JUU SANA.

Linapokuja suala la ujenzi mambo hayako tofauti kwani kunahitajika wataalamu wa fani za ujenzi wa usanifu majengo na uhandisi mihimili kuhusika katika kusimamia, kukagua na kudhibiti ubora katika miradi ya ujenzi.

WATAALAMU WA USANIFU MAJENGO NA UHANDISI MIHIMILI NDIO WAAMUZI WAKUU WA UBORA NA VIWANGO VYA MRADI WA UJENZI.

Lakini miradi ya ujenzi mingi ya ukubwa wa kawaida hukabidhiwa kwa wakandarasi ambao wengi sio wa taaluma husika na mara nyingi utakuta ndio wenye maamuzi ya mwisho au ndio wanaoamua mwelekeo na ubora wa viwango vya mradi husika. Lakini kwa sababu hawana utaalamu au sio wabobezi wa taaluma husika maamuzi yao huwezi kuathiri ubora wa mradi au kusababisha uharibifu kabisa, hivyo kila mkandarasi ambaye sio mtaalamu wa fani yoyote ya ujenzi anapaswa kuwa na wataalamu wa fani hizo katika kila hatua wanayohusika.

MKANDARASI YEYOTE ASIYE NA TAALUMA YA UJENZI ANALAZIMIKA KUWA NA WASHAURI WA KITAALAMU WA TAALUMA ZA UJENZI KWA KILA MRADI WA UJENZI ANAOFANYA IKIWA ANAHITAJI UWE KATIKA VIWANGO VYA JUU VYA UBORA.

Miradi mingi ya ujenzi mikubwa iliyoharibika au kufanyika chini ya viwango au hata kuharibu ile picha ya nje ya muonekano wa jengo husababishwa zaidi na ukandarasi ambao unashindwa kuzingatia aidha ushauri wa wataalamu au hakuna kabisa washauri wa kitaalamu katika mradi husika. Ukifanya ziara ya kutembelea maeneo mengi ya ujenzi utakuta mambo mengi yanaharibika kwa sababu mambo mengi yanafanyika bila kuzingatia utaalamu wa fani za ujenzi.

MIRADI MINGI YA UJENZI ILIYOJENGWA CHINI YA VIWANGO AU KUHARIBU MUONEKANO WA NJE NI ILE AMBAYO MKANDARASI AMESHINDWA KUHUSISHA WATAALAMU WA TAALUMA HUSIKA.

Architect Sebastian Moshi

Whatsapp/Call +255717452790.

1 reply

Leave a Reply

Want to join the discussion?
Feel free to contribute!

Leave a Reply to Aliko Musa Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *