Entries by Ujenzi Makini

TATIZO LA RAMANI ZA NYUMBA ZA KWENYE MITANDAO.

Kumekuwepo na uuzwaji wa ramani za nyumba mbalimbali za mitandaoni hasa miaka hii ya karibuni na baadhi ya watu wamekuwa wakishawishika kununua kwa sababu zinaonekana zinapatikana kwa bei rahisi kidogo pia. Lakini matatizo yanayoletwa na ramani za mitandaoni ni makubwa sana kiasi kwamba hata huo urahisi wa bei hutaona umuhimu wake tena. Jambo moja la […]

MUONEKANO BORA WA NYUMBA YA KISASA PEKEE HAUTOSHI

Kutokana na mapinduzi makubwa kisanifu na kiteknolojia katika ujenzi na hasa katika taaluma ya ujenzi vilivyopelekea kuongezeka kwa ubunifu muonekano wa majengo ya kisasa umekuwa ni wenye kuvutia sana na kila moja kuweza kuwa wa kipekee pasipo kufanana sana kwa kila mradi. Jambo hili limepelekea watu kuvutiwa sana na muonekano na kuweka akili zao zaidi […]

NYUMBA ZA KISASA ZINAHITAJI MAANDALIZI NA MWONGOZO WA KITAALAMU KATIKA UJENZI

Ili mtu aweze kuipenda nyumba yake na kufurahia kila anapoitazama inapaswa kuwa ni nyumba nzuri inayomvutia angalau yeye binafsi. Na hii ndio sababu watu wengi wamekuwa wakivutiwa sana na aina mbalimbali za nyumba za kisasa za wakati huu ambazo zimekuwa na mwonekano na mvuto wa kipekee kutokana na mapinduzi makubwa ya kisanifu yanayoendelea sambamba na […]

KAMPUNI ZA UJENZI TANZANIA ZINAPASWA KUWA NA WASHAURI WA KITAALAMU.

Wote tunafahamu kwamba nchi yetu ina uhaba mkubwa sana linapokuja suala la washauri wa kitaalamu katika sekta mbalimbali. Sekta ya ujenzi ni kati ya maeneo ambayo washauri wa kitaalamu wamekuadimika sana kwenye miradi ya ujenzi, jambo linalopelekea kushuka sana kwa ubora na thamani ya miradi ya ujenzi ukilinganisha na thamani ya fedha iliyotumika kwenye miradi […]