Entries by Ujenzi Makini

ENEO LA BUSTANI NYUMBANI, NYUMBA YAKO SIO KARAKANA.

Katika suala zima la ujenzi, hasa ujenzi wa makazi watu wamekuwa wakiweka umakini mkubwa zaidi kwenye ujenzi wa jengo la nyumba na kuweka umakini kidogo sana kwenye mandhari inayoizunguka nyumba kitu kinachopelekea kukosekana kwa umakini wa kimpangilio. Jambo muhimu sana la kuzingatia ni kwamba makazi ya kuishi ni eneo linalotakiwa kuwa na mandhari bora yenye […]

NI BORA KUJIKUSANYA UKAJENGA NYUMBA YAKO TARATIBU KULIKO KUHARAKISHA NA KULIPUA

Binadamu kiasili tumeumbwa kuvutiwa na kutamani matokeo ya mwisho wa jambo lolote bila kujali mchakato wake ulivyoenda, ambapo mtazamo huu umekuwa ukiongezea nguvu na msemo wa kiingereza unaosema, “the end justifies the means” ikimaanisha mwisho wa kitu ndio huweza kuelezea mchakato wake, yaani ilimradi tu ufike mwisho kisha njia uliyopitia au mchakato utajieleza wenyewe baada […]

KUTUMIA GHARAMA KUBWA PEKEE HAITOSHI, UJENZI BORA UNAHITAJI UTAALAMU SAHIHI.

Imekuwa ni jambo la kusikitisha sana mtu unapokutana na majengo mbalimbali ya makazi, biashara, taasisi mbalimbali, ofisi, viwanda n.k., na kukutana na majengo makubwa ambayo yamegharimu fedha nyingi sana kujengwa lakini yakiwa na ramani za viwango duni sana. Hili linasikitisha sana kwa sababu unaona wazi kwamba fedha iliyotumika kujenga ni kubwa sana na ilihitajika kutolewa […]

WEKA MPANGILIO SAHIHI WA KIMATUMIZI KATIKA KIWANJA CHAKO KADIRI YA UTAMADUNI WAKO NA MAHITAJI YAKO.

Mpangilio wa kimatumizi ni eneo muhimu sana la kulifanyia kazi kwa ukaribu, umakini na uangalifu pale unapokuwa unatengeneza michoro ya ramani kwa ajili ya nyumba yako ya kuishi. Mara nyingi watu wamekuwa wakimwachia mtaalamu wa usanifu kuamua namna atapangilia mwenyewe kadiri anavyofikiri inafaa kitaalamu bila kujua kwamba anayeenda kutumia eneo hilo sio mtaalamu bali ni […]

MUDA WA ZEGE KUMWAGILIWA MAJI(CURING) KATIKA JENGO NI ANGALAU SIKU 21.

Katika ujenzi hususan wa majengo, mifumo yote inayohusika na mihimili ya jengo hutumia zege ikiwa jengo husika halijatumia mihimili ya chuma. Hata hivyo majengo yanayojengwa kwa chuma ni machache sana ukilinganisha na majengo yanayojengwa kwa zege. Hivyo majengo mengi katika mifumo yake ya mihimili yaani nguzo(columns), maboriti(beams), zege ya sakafu(slabs) na ngazi hujengwa kwa kutumia […]

TOVUTI YETU YA UJENZI MAKINI NI KWA AJILI YA KUJIFUNZA KWA MAELEZO NA PICHA.

Katika tovuti yetu ya ujenzi makini tumekuwa tukiandika makala nyingi za aina mbalimbali kuanzia makala za kitaalamu, kiufundi, miongozo, maelekezo, ushauri n.k. Lakini pia tumekuwa tukiambatanisha na uhalisia katika picha ya vitu mbalimbali japo sio picha zote huendana na ujumbe moja kwa moja lakini angalau picha hizi huweza kujenga hamasa na kumjengea msomaji picha ya […]