Entries by Ujenzi Makini

NYUMBA YA NDOTO ZAKO.

Karibu kila mtu kwenye maisha huwa na nyumba ya ndoto zake, hasa watu wanapokuwa katika umri mdogo kila mmoja huota kwamba atakuja kuishi kwenye nyumba fulani na mara nyingi nyumba hiyo huwa ni kubwa na ya kifahari sana. Kwa uzoefu wangu ni watu wachache ambao hufikia ndoto hii mapema kadiri ya ndoto zao. Watu wengi […]

UNAWEZA KUBADILISHA NYUMBA YAKO KUWA GHOROFA

Uwezo wa mtu kiuchumi mara nyingi huwa unaendelea kukua kutokea chini kwenda kwa sababu muda nao ni moja ya sababu za kipato cha mtu kuongezeka ikiwa mtu huyo anafuata kanuni sahihi za mafanikio. Watu wengi hujenga nyumba zao za kuishi au hata aina nyingine za nyumba kadiri ya kipato chao kinavyoruhusu kwa wakati husika, lakini […]

KUFANYA UKARABATI WA JENGO AU KUONGEZA UKUBWA NA KUJENGA HUSISHA MTAALAMU.

Mara kwa mara watu wamekuwa wakifanya ukarabati wa majengo au nyumba zao kwa sababu mbalimbali zikiwemo uchakavu, uharibifu au pale wanapotaka kubadili matumizi au kuboresha jengo lenyewe. Lakini zaidi watu wamekuwa wakiliongeza jengo pia kwa sababu mbalimbali zikiwemo kubadili matumizi, kuongeza matumizi, kukarabati jengo walilonunua kutoka kwenye matumizi ya makazi kwenda kwenye matumizi ya biashara, […]

KATIKA UJENZI BORA, GHARAMA ISIWE KIKWAZO.

Katika ujenzi karibu mara zote makosa huwa yanatokea ambapo inategemea endapo hakutakuwa na ukaguzi wa mara kwa mara makosa huweza kuwa mengi na gharama ya kuyarekebisha kuwa kubwa lakini kunapokuwepo na ufuatiliaji wa karibu wa mara kwa mara makosa hupungua na gharama ya kuyarekebisha kupungua pia. Ni muhimu sana kuwepo kwa mtaalamu wa kufanya ukaguzi […]

KWA MRADI WA UJENZI UNAOENDESHWA BILA KUFUATA UTARATIBU ULIOWEKWA NA MAMLAKA HUSIKA KISHERIA INAPASWA AWEPO MTU WA KUFANYA MAAMUZI YA MWISHO.

Wote tunajua kwamba mamlaka za ujenzi zimeweka utaratibu unaotakiwa kufuatwa katika miradi ya ujenzi mpaka kufikia mtu mwenye maamuzi ya mwisho kabisa katika ujenzi pale inapokuwa inatakiwa. Kwa kawaida maamuzi mengi ya ujenzi na hasa ya kitaalamu hufanywa na mshauri wa kitaalamu wa eneo husika(consultancy) na kama hayupo basi atafanya msaidizi wake au mtu mwingine […]

ATHARI ZA KIMAZINGIRA ZA MRADI WA UJENZI.

Mradi wowote wa ujenzi huja na athari zake kimazingira kulingana na aina ya mradi husika. Athari zinatofautiana viwangoa mabpo kuna miradi mingine huja na athari hasi kidogo sana na mingine huja na athari hasi nyingi zaidi na kadiri mradi unapokuwa na athari nyingi sana hasi ndivyo kadiri unavyozidi kupoteza uhalali wa kuwa katika eneo husika […]

WATU WANAOHUSIKA KUFANYA MAAMUZI KWENYE MRADI WA UJENZI

Kutokana na kutokufahamu taratibu na madhara yanayoweza kusababishwa na ufanyaji wa maamuzi kiholela kwenye mradi wa ujenzi, imekuwa jambo la kawaida kwa watu kujifanyia maamuzi kwenye mradi wa ujenzi vile watakavyo. Hili limekuwa linakuja na gharama kubwa kwa sababu watu hawa wamekuwa wakifanya maamuzi wakiwa hawana taarifa za kutosha wala uzoefu na utaalamu wa jambo […]