Entries by Ujenzi Makini

CHANGAMOTO KARIBU ZOTE ZA KWENYE JENGO ZINATATULIKA.

Majengo kama ilivyo katika maeneo mengine yote na kwenye fani zote huwa yanachakaa na mitindo yake pia kupitwa na wakati kadiri miaka inavyozidi kwenda mbele na mabadiliko zaidi. Katika tasnia ya usanifu majengo na ujenzi mabadiliko ya kiteknolojia yanayopelekea mitindo mipya ya majengo pamoja na vifaa vya ujenzi yameathiri sana tasnia hii hususan kwa namna […]

NAMNA NZURI NA YA UHAKIKA YA KUTENGENEZA ARCH (NUSU DUARA) ZA UREMBO KWENYE MAJENGO.

Nimekuwa nikitembelea majengo mbalimbali yaliyojengwa na yanajengwa katika kufanya ukaguzi au kutoa ushauri kuhusu ujenzi na kukutana na changamoto na makosa mbalimbali. Makosa mengi yanatokana aidha na ujinga yaani ile mtu kushindwa kujua afanye nini katika eneo husika la ujenzi au uzembe yaani pale mtu unakuta anajua cha kufanya lakini kwa sababu mbalimbali ikiwemo tamaa […]

MALIPO YA MAFUNDI NA VIBARUA KWENYE MRADI WA UJENZI NI KWA KAZI AU KWA SIKU?

Katika kuhakikisha kwamba miradi ya ujenzi inafanyika kwa ubora na kwa gharama nafuu zaidi kumekuwa na mbinu mbalimbali za kushughulika nayo katika utekelezaji ikiwemo usimamizi na udhibiti wa ufundi na mafundi. Kumekuwa na utofautiano kwamba ni njia ipi sahihi ya kuwalipa mafundi ambayo inafanya kazi vizuri zaidi na inayoweza kusaidia kwa uhakika kupunguza gharama na […]

CHANGAMOTO ZISIZOTARAJIWA KWENYE UJENZI.

Moja kati ya changamoto kubwa ambayo mara nyingi huwa tunakutana nayo kwenye ujenzi ni kukutana na changamoto usiyoitarajia. Changamoto zisizotarajiwa hutokea wakati wowote na kuleta usumbufu mkubwa na wakati mwingine hata hasara kwa sababu inaweza kuwa ni changamoto ambayo utatuzi wake unakuwa sio rahisi. Changamoto hizi tunapokutana nazo zinayumbisha sana mradi wa ujenzi kwa sababu […]