Entries by Ujenzi Makini

CHANGAMOTO ZA MATUMIZI YA KIWANJA

Watu wengi wamekuwa wakikutana na changamoto za kusumbuliwa na mamlaka hasa halmashauri za miji, manispaa na majiji pale wanapokuwa wanafuatilia vibali vya ujenzi kutokana na suala zima la kigezo cha matumizi ya kiwanja. Mara nyingi hasa miaka ya hivi karibuni kupata kibali cha ujenzi wa eneo lako suala la matumizi ya kiwanja limekuwa ni changamoto […]

GHARAMA ZA UJENZI ZINAJUMUISHA MICHORO YA RAMANI

Watu wengi wanapofikiria kuhusu gharama za ujenzi huanza kufikiria wakati wa kujenga, yaani kuanzia kwenye kuchimba msingi huku gharama za michoro ya ramani wakizitenganisha na ujenzi wenyewe. Jambo hili limekuwa na madhara kadhaa na limekuwa likiwaumiza wataalamu wa ujenzi na likimuumiza hata na mteja mwenyewe pia kwa sababu huwa na madhara yafuatayo. Kwa taratibu zilizowekwa […]

DAFTARI LA MAELEKEZO(INSTRUCTION BOOK)

Katika eneo la ujenzi(site) mambo huwa ni mengi sana na maamuzi yanayopelekea mabadiliko mbalimbali hufanyika mara kwa mara sana kiasi kwamba kama maamuzi hayo hayajawekwa kwenye maandishi ni rahisi baadhi ya mambo kusahaulika hivyo kutoingizwa kwenye utekelezaji kwa usahihi kama ilivyoamuliwa na matokeo yanayokusudiwa kushindwa kufikiwa. Hivyo ni muhimu sana kuwepo kwa daftari la maelekezo […]

VIKAO VYA KWENYE ENEO LA UJENZI(SITE MEETINGS)

Kwa mujibu wa taratibu zilizowekwa na mamlaka husika, kila mradi wa ujenzi hutakiwa kuwa na vikao vya mara kwa mara kwa ajili ya kujadili maendeleo ya mradi kuanzia masuala ya kiufundi ya kazi, fedha, ratiba ya kazi juu ya muda uliopangwa, mabadiliko, maamuzi mbadala pamoja na changamoto nyingine zinazoweza kuwa zinaukabili mradi husika. Vikao hivi […]

BILA KUFUATILIWA NA MSIMAMIZI MTAALAMU, KAZI YOYOTE YA UJENZI ITAHARIBIKA.

Katika kitu ambacho hutokea karibu mara zote katika mradi wa ujenzi ni pamoja na mabadiliko ya jengo wakati wa kujenga ambayo yanaleta utofauti kidogo na michoro ya mwanzo iliyokusudiwa. Mabadiliko hutokea mara zote na siku zote, wakati mwingine yakisababishwa na changamoto zilizojitokeza wakati wa ujenzi na wakati mwingine yakisababishwa na maamuzi ya mteja mwenyewe baada […]

KUFANIKISHA UJENZI BORA EPUKA KUTUMIA HISIA, ANGALIA MANUFAA.

Mara nyingi sisi binadamu tuna udhaifu wa kuongozwa na hisia zaidi na kutoona uhalisia jambo linalopelekea kufanya maamuzi yasiyo sahihi mara nyingi zaidi kuliko maamuzi sahihi na mwishoni tunaishia kujutia na kusema laiti ningejua, watu wachache ambao wamejaliwa kutumia akili na maarifa zaidi kuliko hisia wamekuwa wanashinda zaidi kuliko wengi wanaoongozwa na hisia. Changamoto ni […]

KUEPUSHA KUHARIBU KAZI, MPE MTAALAMU UHURU WA KUTOSHA

Mara nyingi kama wewe ni mteja mtaalamu wa kufanya jengo huwa anakusikiliza unataka nini na kufanya unachotaka kwa sababu lengo lake ni kukuridhisha wewe na kufanya unachotaka kwa sababu wewe ndiye unayelipa pesa na mwisho wa siku wewe ndiye mmiliki wa jengo husika. Changamoto huwa inatokea pale mteja ndio anakuwa mpangaji na mwamuzi wa kila […]

UKUBWA WA NYUMBA UNATOKANA NA UKUBWA WA VYUMBA NDANI YA NYUMBA

Imekuwa kawaida kukutana na mteja anakwambia nahitaji nyumba iwe na vyumba vikubwa ndani vyenye ukubwa wa kutosha, anakwambia “nataka sebule kubwa na master bedroom kubwa” lakini mwisho anaishia kukwambia lakini nyumba yenyewe isiwe kubwa, kwa sababu anataka nyumba ambayo haitamgharimu sana fedha nyingi kuijenga. Kwanza kabisa nakubali kwamba kadiri nyumba inavyokuwa kubwa ndivyo kadiri gharama […]