Entries by Ujenzi Makini

UJENZI WA NYUMBA KIJIJINI.

Watu wengi hasa katika nchi zinazoendelea ni aidha wa wametokea vijiji au wazazi wao walitokea vijijini hivyo wana makazi ya kurithi katika maeneo ya vijijini. Sasa kutokana na uhalisia huo watu wengi wamekuwa wakisukumwa kujenga nyumba za kuishi katika maeneo waliyotokea hata kama hawaishi maeneo haya kwa muda wote wakiwa na sababu mbalimbali. Kuna wengine […]

MRADI WA UJENZI USIOENDESHWA KWA MFUMO.

Kabla ya kujadili namna ya kuendesha mradi wa ujenzi bila mfumo au pamoja na mfumo kwanza tujadili mfumo ni nini? Mfumo maana yake ni utaratibu fulani uliopangwa ambao unafuata mchakato maalum katika ufanyaji wa mambo yake kwa kufuata mfululizo fulani uliopangiliwa. Mchakato unaofuatwa katika mfumo husika mara nyingi huwa na hatua au vitendo vinavyojirudia rudia […]

CHANGAMOTO YA KUKOSEKANA KWA MSANIFU MAJENGO KWENYE MRADI WA UJENZI.

Kama tulivyojadili mara nyingi sana katika makala zilizopita kwamba kuna mapungufu mengi sana hujitokeza katika miradi ya ujenzi kwa sababu ya kukosekana kwa wataalamu husika wa ujenzi huo. Ikiwa mtaalamu kamili hatatumika kuanzia hatua ya michoro mpaka mwisho basi jengo litakuwa na mapungufu makubwa sana kuanzia ya kimatumizi mpaka kimuonekano. Na ikiwa mtaalamu atahusika katika […]

MRADI WA UJENZI UNAHITAJI MAANDALIZI MAKINI SANA KABLA ILI KUEPUKA USUMBUFU BAADAYE.

Ni wazi kwamba kwa mtu yeyote ambaye amewahi kujenga na kusimamia ujenzi wake mwenyewe anajua ni jinsi gani mradi wa ujenzi unavyoambatana na changamoto na usumbufu mkubwa wakati wa utekelezaji wake hasa kama hakukuwa na maandilizi na mikakati madhubuti mwanzaoni. Katika usumbufu huu kitu ambacho hugharimu sana ni muda ambao mradi huo unachukua katika kufuatilia […]

KWENYE UJENZI UFUNDI NA USIMAMIZI WA KITAALAMU NI VITU VIWILI TOFAUTI.

Baadhi ya watu wamekuwa hawaelewi sana undani wa yale yanayoendelea kwenye miradi ya ujenzi hivyo wamekuwa wakidhani kwamba wakishakuwa na fundi wa kuwajengea nyumba yao basi wanakuwa wamemaliza suala la ujenzi kwa uhakika kabisa. Lakini unapokuja kwenye uhalisia wa kazi unakuta hilo sio kweli kwani hata katika ujenzi unaozingatia taratibu rasmi zilizowekwa na mamlaka zinazosimamia […]

MAAMUZI KWENYE UJENZI YANAHITAJI BUSARA NA AKILI.

Kwa kawaida sisi binadamu huwa tuna njia mbili tunazotumia kwenye kufikia maamuzi ambazo ni kufanya maamuzi kwa kutumia hisia au kufanya maamuzi kwa kutumia akili. Njia ya kufanya maamuzi kwa kutumia hisia huwa ndio njia rahisi inayokuja yenyewe kwa haraka na ndio yenye nguvu kwa watu wengi sana. Hata hivyo wanasaikolojia wengi wanaamini kwamba binadamu […]