Entries by Ujenzi Makini

UKIFANYA MAAMUZI KWENYE UJENZI KIENYEJI UTAICHUKIA NYUMBA YAKO.

Baada ya hatua ya michoro ya ramani kukamilika kisha mradi wote unaoenda kufanyika kuwa wazi, watu wote wanategemea kuona utekelezaji wa mradi huo ambao unaunda kufanyika kama jinsi michoro ya ramani inavyoonyesha. Mteja na wadau wengine wanakuwa wameliona jengo na uzuri wake na hivyo wanatarajiwa mwishoni kuona kile kilichofanyika kwenye michoro. Na kweli kazi ikifanyika […]

MSIMAMIZI WA UJENZI AONYESHE MAJUKUMU YAKE NA KUTOA RIPOTI YA KAZI YAKE.

Katika miradi ya ujenzi iwe mteja ameweka mkandarasi kamili au msimamizi peke yake, yule msimamizi aliyewekwa anapaswa kufanya kazi inayoeleweka na kupimika. Yaani msimamizi au mkandarasi anapaswa kupeleka mpango wake mzima wa kazi ambayo anaenda kuifanya tangia mwanzo mpaka mwisho. Mpango kazi huo utaonyesha majukumu yake anayokwenda kufanya na matokeo yanayotegemewa sambamba na muda anaokwenda […]

MABADILIKO YOYOTE YASIYOMHUSISHA MTAALAMU KATIKA MRADI WA UJENZI YANAHARIBU.

Wiki iliyopita nilienda kutembelea eneo moja la ujenzi wa ghorofa ya mtu Dar es Salaam ambayo nilifanya michoro na kuacha msimamizi wa ujenzi maarufu kama “Site Foreman” akiendelea na kazi ya kusimamisha jengo hilo. Kisha nilirudi tena mwisho wa wiki iliyofuata wakati wanaanza kazi ya kupangilia vyumba kwa ajili ya kuhakikisha hakutokea makosa yoyote katika […]

MRADI WA UJENZI UKIKOSA USIMAMIZI SAHIHI LAZIMA KUNA KITU KITAHARIBIKA.

Katika maisha hakuna kitu kigumu kama kutabiri mambo yatakayotokea kwenye jambo lolote ambayo hayaonekani katika hali ya kawaida. Mara nyingi mtu anapowaza jambo lolote ambalo linahusisha mchakato fulani kwenye utekelezaji wake huwa anawaza kwa kudhania kwamba kila kitu kitafanyika kwa usahihi na uhakika bila hata kujali uwezo, umakini na mwongozo walionao watendaji wa mradi husika. […]

UTAALAMU WA KUCHORA NA KUJENGA NYUMBA YOYOTE NDIO UNAOTUMIKA KWENYE KUCHORA NA KUJENGA NYUMBA/JENGO LINGINE LOLOTE.

Mara kwa mara nimekuwa nikikutana wateja mbalimbali wenye mahitaji tofauti tofauti ya kila namna. Licha ya kwamba mahitaji haya yamekuwa yakija kwa upekee tofauti tofauti kuna kitu kimoja kimekuwa kikinishangaza na kuleta usumbufu kidogo. Jambo hilo ni wateja kuamini kwamba mtalaamu anatakiwa awe alishafanya jengo la aina fulani ili kuwaza kufanya mradi wake huo. Ingawa […]

KWENYE UJENZI USIPOKEE USHAURI AMBAO HUJAOMBA.

Kwa asili sisi binadamu tuna tabia ya kisaikolojia ya kurithi ambapo huwa tunawamaamini zaidi watu wetu wa karibu au watu ambao tuna mahusiano nao ya karibu kuliko watu wa mbali tusiowajua au kuwa na ukaribi nao. Yaani tumeumbwa kwamba wale watu ambao tuna mahusiano ya karibu na ya kina huwa tunaamini zaidi kile wanachotuambia na […]