Entries by Ujenzi Makini

ELEWANA NA VIONGOZI WA SERIKALI YA MTAA JUU YA KIWANJA CHAKO KABLA HUJAANZA KUJENGA.

Kama kuna mambo yanayoendelea ambayo huyajui kuhusu kiwanja chako utashangazwa jinsi yatakavyojitokeza mara utakapoamua kujenga. Baadhi ya viwanja huwa vinauzwa vikiwa na utata au kukiwa bado kuna changamoto ambazo hazijatatuliwa kuhusiana na viwanja hivyo. Lakini huwa hakuna namna ya kutatua au wakati hata wahusika unakuta hawana taarifa yoyote ya kinachoendelea juu ya kiwanja husika mpaka […]

UKITAKA KAZI IFANYIKE KWA HARAKA NI MUHIMU PANDE ZOTE KUWAJIBIKA.

Kati ya vitu ambavyo huwaweka njia panda washauri wa kitaalamu pamoja na watu wengine ambao wanatoa huduma za ujenzi basi kinachoongoza huwa ni malipo. Ukiachana na uhalisia kwamba malipo huweza kulipwa kidogo lakini wakati mwingine malipo hucheleweshwa na wakati mwingine kutolipwa kabisa. Suala hili limepelekea watu kupoteza imani katika kazi kwenye suala la malipo na […]

GHARAMA ZA UJENZI NI MACHAGUO YAKO MWENYEWE.

Gharama za ujenzi zimekuwa ni sehemu nyeti na muhimu sana kwa watu kufanya maamuzi juu ya miradi yao ya ujenzi kuanzia mwanzo kwenye kuandaa michoro mpaka kujenga kwa maana ya kuanzia kwenye huduma za ushauri wa kitaalamu, huduma za ujenzi mpaka vifaa vya ujenzi. Watu wamekuwa wakiogopa sana gharama hizi na kuweka umakini mkubwa kwenye […]

UJENZI WA NYUMBA NI SAFARI KWA VIJANA WALIO WENGI.

Kila kijana aliyefikisha umri wa kuanza kujitegemea hutamani kuwa na nyumba ya kuishi ambayo kwa watu wengi pia huwa ni ndoto yao ya miaka mingi tangu utotoni. Lakini tofauti na miaka ya zamani sana ambapo kujenga nyumba ilikuwa ni suala la kutumia teknolojia na malighafi zilizopo katika mazingira husika kwa usaidizi pia familia pamoja na […]

CHANGAMOTO NI UFUATILIAJI MADHUBUTI KUTOKA KWENYE MAMLAKA ZA UJENZI.

Kwa mujibu wa utaratibu uliowekwa na mamlaka za ujenzi, huwa kuna ufuatiliaji wa mara kwa mara wa miradi mbalimbali inayoendelea kuhakikisha inafuata taratibu zote sambamba na kuzingatia kutekeleza kwa usahihi michoro ambayo imepitishwa na mamlaka na kupatiwa kibali. Utaratibu huu huweza kusaidia katika kuhakikisha kwamba kazi husika inafanyika kwa usahihi na kwa viwango kwa namna […]

KAZI YA UJENZI IWE NA MTAALAMU WA KUIKAGUA NA KUIDHINISHA.

Kwa miradi mikubwa ambayo inafuata taratibu zote za kitaalamu zilizowekwa na mamlaka husika hii sio changamoto kubwa kwa sababu mfumo wa kufanya kazi kitaalamu unafuatwa kwa usahihi na hivyo kudhibiti changamoto zote zinazoweza kusababishwa na udhaifu wa kimfumo. Lakini kwa miradi isiyofuata utaratibu wa kufanya kazi kitaalamu uliowekwa na mamlaka husika ambayo mingi ni miradi […]

“USIPOZIBA UFA UTAJENGA UKUTA”, VIKAO NI MUHIMU SANA KATIKA MRADI WA UJENZI.

Kuna huu msemo maarufu wa kiswahili unaosema “usipoziba ufa, utajenga ukuta” ni msemo ambao una umuhimu mkubwa kwenye baadhi ya maeneo na hapa tunaona ukiingia kwenye hili eneo la ujenzi. Katika mradi wowote wa ujenzi vikao vya kuhusu maendeleo ya mradi husika ni muhimu sana katika kuepuka kuingia kwenye changamoto kubwa au hasara kubwa. Tunafahamu […]